Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania

TLSB Logo TLSB Logo
Tafuta kwenye kwa

Majukumu

Majukumu ya Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania yanatekeleza matakwa ya sheria ya Bunge Namba 6 ya mwaka 1975. Majukumu hayo ni:

  1. Kuanzisha, kuendesha, kuongoza, kuboresha, kutunza na kuendeleza Maktaba za umma kote nchini kuanzia ngazi za mikoa, wilaya hadi tarafa.
  2. Kuupatia umma wa Watanzania taarifa mbalimbali zilizokusanywa kutoka katika ulimwengu mpana wa maarifa kwa ajili ya elimu, utafiti na maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.
  3. Kukusanya na kuhifadhi machapisho ya kitaifa.
  4. Kutoa mafunzo na kuendesha mitihani ya taaluma ya Ukutubi kwa wafanyakazi wa Bodi, Maktaba za shule, vyuo na taasisi mbalimbali nchini.
  5. Kuanzisha, kukuza, kusimamia, kuratibu na kuendeleza huduma za maarifa na utafiti (documentation services) nchini.
  6. Kutoa ushauri na uelekezi kwa idara za serikali, taasisi na mashirika mengine kuhusu kuanzisha, kuendeleza na kuboresha huduma za Maktaba katika maeneo yao.
  7. Kuendesha mfumo wa ushirikiano kati ya Maktaba za Umma na Taasisi nyingine zinazotunza nyaraka ili kuwawezesha wananchi kupata taarifa kwa gharama nafuu.