Pichani: Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Elimu) Dkt. Hussein Mohamed Omar (aliyekaa katikati) katika picha ya pamoja na Menejimenti ya TLSB mara baada ya kufanya ziara ya kiofisi katika ofisi za Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB) Makao Makuu Dar es Salaam, tarehe 22 Julai, 2025. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa TLSB Dkt. Mboni Ruzegea na Kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa WyEST Ndug. Sebastian Inoshi.
Pichani: Menejimenti ya TLSB na Maktaba ya Jamii Bustani, Rombo Kilimanjaro, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kikao maalum kilichofanyika tarehe 31 Julai, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano TLSB Makao Makuu Dar es Salaam, kikao hicho ni hatua muhimu kuelekea uzinduzi wa Maktaba hiyo utakaofanyika hivi karibuni. Kutoka Kulia waliokaa ni Ndug. Fidelis Swai Mjumbe wa Menejimenti ya Maktaba ya Bustani, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji Huduma za Maktaba Dkt. Rehema Ndumbaro (Katikati) na kulia ni ndug. Romani Urassa ambaye pia ni Mjumbe wa Menejimenti ya Maktaba ya Jamii Bustani. Waliosimama ni Menejimenti ya TLSB.
TANGAZO: Mkuu wa Chuo cha Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (SLADS) anakaribisha maombi ya kujiunga na Chuo kwa kozi za Ukutubi, Uhifadhi Nyaraka na ICT kwa mwaka wa masomo 2025/2026. Nyote mnakaribishwa!
Bodi ya Wakurugenzi TLSB katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof. Rwekaza Mukandala ( Aliyekaa katikati) baada ya kumalizika kwa mafunzo ya Wajumbe wa Bodi na Menejimenti tarehe 10 Aprili, 2025 katika hoteli ya Ramada, Dar es Salaam.
Kuwa Taasisi ya umma inayoongoza nchini katika kutoa na kusambaza taarifa mbalimbali kwa njia ya vitabu, machapisho na teknolojia ya kisasa kupitia mt...
Kutoa na kusambaza huduma sahihi kwa watu wote kwa wakati muafaka ili kuendeleza kisomo, kujiburudisha na kuendeleza utamaduni kwa jamii. Pia kukusany...
TLSB ni chombo kilichopewa mamlaka ya kisheria ya kupata, kupanga, na kusambaza, taarifa katika nyanja zote za maisha. Maarifa yaliyokusanywa kupitia...
Bodi ya huduma za maktaba Tanzania (TLSB), imepokea vitabu zaidi ya 150 kutoka kwa familia ya marehemu Christopher Mwaijonga ya jijini Dar es salaam, tarehe 6 Februari 2024.
Akimwakilisha Mkurugenz...